TAZAMA NAMI:
Ni vema kuwa na furaha wakati wote, moyo wako uwe unaachilia kicheko, moyo wako uwe unabubujika furaha wakati wote, jiwekee hazina ya kicheko cha nafsi, jiwekee furaha inayoujaliza moyo wako wakati wote, nafsi yako isiwe na kuinama, itie nafsi yako nguvu nyingi wakati wowote.
Na:
Mwl. Samwel Mkumbo
Kuondoa ufahamu ulionao na kukuwekea
ufahamu
mpya juu ya jambo Fulani
Sasa ufahamu mpya unapokuja
ndani yako lengo lake linguine ni kutaka kuondoa ufahamu uliokuwa nao kwanza na
kukuwekea ufahamu mpya kabisa aidha ni sahihi au si sahihi.
Mwanzo 3:4-5 tunasoma hivi;
Nyoka
akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa, kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku
mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu,
mkijua mema na mabaya.
Lakini katika mstari huo pia
kuna kitu natamani nikuoneshe ambacho ni cha msingi sana sana, nacho ni jinsi
shetani anavyoleta ufahamu wake, ufahamu wa shetani unakuja kwa mtazamo ya
kwamba kuna Ukweli mwingi na Uongo kidogo, usidhani ya kwamba shetani kwa kuwa
ni baba wa uongo basi atakuja kukuambia uongo kwa asilimia zote, la hasha!
Lakini anakuja kwa mtindo ambao utaona kuna ukweli mwingi sana.
Angalia vizuri majibu yake
kwa Hawa baada ya kujua Hawa anafahamu nini juu ya hilo alikuja na sentensi
nyingi za Ukweli lakini maneno mawili tu ya Uongo, na anachokifanya shetani
hawezi kuweka msisitizo kwenye yale mengi ambayo huwa ni ukweli, bali anaweka
msisitizo kwenye lile moja au yale machache yaliyo ya uongo.
Angalia huo mstari tena;
Nyoka
akamwambia mwanamke, HAKIKA hamtakufa, kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku
mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu,
mkijua mema na mabaya.
Unaweza kuona ya kwamba pale
penye maneno HAKIKA hamtakufa, ndipo penye uongo lakini ndipo shetani
alipawekea Msisitizo, maana aliweka neno HAKIKA.
Huku kwingine hakuweka
msisitizo wala hakuweka neno HAKIKA AU KWELI kwa sababu alijua ndio ukweli,
sasa alichoweza kufanya ni kuweka msisitizo kwenye lile alilokusudia ambalo ni
la uongo.
Mathayo
2:8
tunasoma maneno haya;
Akawapeleka
Bethlehemu, akasema, Shikeni njia, mkaulize sana mambo ya mtoto; na mkiisha
kumwona, nileteeni habari, ili mimi nami niende nimsujudie.
Hebu tazama kwa makini
maneno aliyoyasema Herode mwanzoni mwa maagizo yake ….mkaulize sana mambo ya mtoto;….. halafu angalia alivyomalizia
sentensi aliyomalizia nayo .,. ili mimi
nami niende nimsujudie……
Sasa msingi wetu tuliuweka
katika kuangalia uhusiano wa nafsi yako au nafsi ya mtu mmoja mmoja inapokuwa
salama na inapokuwa Bora inahusianaje na Uhai wa Kanisa.
MATENDO
20:28 inasema hivi;
Jitunzeni
nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa
waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu
yake mwenyewe.
Na ukiutazama huo mstari kwa
haraka unatupeleka kwenye hali ya kuamini kwamba Paulo alikuwa akisema na
Viongozi, na ndivyo inatuonesha mistari inayotangulia mstari huo, hasa mistari
miwili yaani wa 17-18.
Lakini nataka niweke jambo
moja ndani yako ya kwamba ile tu mistari hiyo kuwekwa kwenye maandiko basi kwa
namna moja inatuhusu na sisi, sasa nataka nikutazamishe jambo moja la msingi
kidogo kutoka kwenye mstari ule wa 28. Hebu tuusome tena mstari huo;
Jitunzeni
nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa
waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu
yake mwenyewe. MATENDO 20:28.
Sasa hebu tuanzie na maneno
yale Jitunzeni nafsi zenu,….. yaani
Jihifadhini, Jilindeni, Jiwekeni Salama nafsi zenu,….halafu weka maneno haya ,…mpate kulilisha kanisa lake Mungu,…
Lakini maneno yaliyonipa
Nguvu kuweka mstari huu kama msingi na kuutazama si kama mstari unaowahusu
wazee wa kanisa, au wachungaji tu, au maaskofu tu, au wahubiri au watu wenye
vyeo vya aina Fulani katika kanisa ni yale maneno yanayosema hivi; …ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa
waangalizi ndani yake….
Ni ngumu kuelewa kwanini
neno hili WAANGALIZI lina umuhimu sana katika mstari huu, na ndilo
linalotufanya tujifunze umuhimu wa kuzitunza nafsi zetu kwa ajili ya uhai wa
kanisa, neno Mwangalizi wakati mwingine linatumika kama Askofu, yaani
mwangalizi.
TAZAMA NAMI:
Neno askofu kwa utaratibu wa
cheo ni MCHUNGAJI WA WACHUNGAJI, lakini kwa utaratibu wa Wokovu na Kiroho ni
mtu yeyote ambaye Nafsi yake AMEIUNGANISHA na Kanisa ya kwamba yupo kuhakikisha
kila jambo linalotakiwa kwenye kanisa linaenda kama itakiwavyo, aidha kwa
maombi yake au kwa mali zake.
Tito
1:7
tunasoma maneno haya;
Maana
imempasa askofu awe mtu asiyeshitakiwa neno ,kwa kuwa ni wakili wa MUNGU; asiwe
mtu wa kujipendeza nafsi yake,asiwe mwepesi wa hasira,asiwe mlevi wala
mgomvi,asiwe mpenda mapato ya aibu.
Sasa kutoka kwenye mstari
huo nataka tuweke mambo kadhaa ambayo ni ya msingi sana kuyaelewa ambayo
ukiyaangalia kwa jicho la ndani utagundua ya kwamba ASKOFU ni mtu wa aina gani,
na maneno yenyewe ni yale yanayotoa sifa za Askofu…
….asiwe
mtu wa kujipendeza nafsi yake, asiwe mwepesi wa hasira, asiwe mlevi wala
mgomvi, asiwe mpenda mapato ya aibu.
Ukitazama hizo sifa za Askofu
utagundua ndizo sifa anazotakiwa kuwa nazo kila mtu aliye ndani ya kanisa, sasa
basi hebu tuunganishe na somo letu uone maana itakayotokea, maana yake kama
tunajua nafsi ya kila mmoja ina umuhimu katika kanisa na ya kwamba kila nafsi
ikiwa Salama na ikiwa Bora basi kuna uhakika wa Kanisa kusimama Imara na kuwa
na Uhai wake.
Waebrania
12:15 tunasoma;
Mkiangalia
sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na
kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.
Uchungu ukiingia nafsini mwa
mtu anayeamini unazaa manung’uniko, na manung’uniko yakiwepo basi kazi ya Mungu
au kama ni kanisa basi haliwezi kuendelea mbele hata kidogo, haijalishi hayo
manung’uniko hayatoki kwa viongozi au yanazalishwa na mtu asiye na nafasi kubwa
kwenye kanisa lakini manung’uniko ni matokeo ya jeraha ya nafsi.
TAZAMA NAMI:
Manung’uniko au maumivu
yanayotoka kwa watu walio ndani ya kanisa au watu wanaoliongoza Kanisa au hata
Familia yana sumu mbaya sana kuliko kitu chochote maana yanaleta hali ambayo
mioyo ya watu inakosa kicheko, na hakuna kitu kibaya moyo ukikosa kicheko, moyo
ukikosa furaha, unaweza ukawa unakula lakini hauna afya nzuri kwa sababu ndani
ya moyo hakuna kicheko, unaweza ukawa unacheka mdomoni lakini moyoni hakuna
kicheko hivyo umebeba majeraha ya uchungu ndani yako.
Ogopa fellowship ambayo watu
wana uchungu, nafsi zao zimeharibika, hata kama ni watoto walio ndani ya
kanisa, au hata kama ni mtu asiye na sifa kubwa ndani ya familia yako lakini
angalia nafsi yake isije kubeba uchungu,
Ni vema kuwa na furaha
wakati wote, moyo wako uwe unaachilia kicheko, moyo wako uwe unabubujika furaha
wakati wote, jiwekee hazina ya kicheko cha nafsi, jiwekee furaha inayoujaliza
moyo wako wakati wote, nafsi yako isiwe na kuinama, itie nafsi yako nguvu
nyingi wakati wowote.
Jisemee moyoni mwako hata
kama hatuli vizuri nyumbani hata kama hatukai kwenye sofa hata kama kanisani
kwetu hakuna vyombo vya mziki, hata kama watoto wangu hawana nguo mpya katika
msimu huu wa sikukuu, hata kama ninaona wenzangu wanabadilisha magari au
wanabadilisha nguo kila ibada au hata kama wapo watu wasiookoka wana fedha
kuliko nilivyo mimi au wana nyumba nzuri kuliko ya kwangu lakini bado nafsi
yangu itakuwa na furaha maana nimepata cha thamani kuliko vyote nimepata
mmiliki wa vyote,,, YESU KRISTO, MUNGU WA KWELI, YEYE ALIYE UZIMA,,, Naaam
nitajilinda NAFSI YANGU maana ninajua uzima wa mtu haupo katika wingi wa vitu
alivyonavyo.
Luka
12:15 inasema hivi;
Akawaambia,
Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu
vyake alivyo navyo.
No comments:
Post a Comment