+255 753 204 743 mkumbosj@gmail.com, facebook.com/mwlsamwelmkumbo

Kuhusu NURU







Huduma  ya  NURU  ni  huduma  isiyofungamana  na  dhehebu  lolote  au tunaweza kusema ni Huduma inayohusisha watu wa Madhehebu yote wanaokiri Wokovu. Ikiwa na msingi wake tangu mwaka 2008. Huduma  ya  NURU  ina  Timu  yenye  watu  16  ndani  yake  ikiwa  na  Viongozi  Watano katika  kusimamia  Utekelezaji  wa  Maono  na  Mipango  ya  huduma.  Ni  Huduma inayoendeshwa  kwa  mtindo  wa  Mafundisho  ya  Neno  la  MUNGU  (Huduma  ya Ualimu)
Kwa  kuwa  Mungu,  aliyesema,  Nuru  itang'aa toka  gizani,  ndiye  aliyeng'aa  mioyoni  mwetu,  atupe  nuru  ya elimu ya utukufu wa Mungu katika uso wa Yesu Kristo (2 Wakorintho 4:6) 
Kwa  ujumla  wake  na  katika  mambo  au  Huduma  zote  zinazofanywa  na  NURU katika  kutenda  kazi  ya  Kueneza  Ufalme  wa  MUNGU,  jambo  la  msingi  tuombalo kwa  BWANA  kwa  unyenyekevu   na  ambalo  tunatamani  MUNGU  atutendee  sisi na wewe pia kwa kuwa ni muhimu ni hili;
…….ATUPE  NURU  YA  ELIMU  YA  UTUKUFU  WA  MUNGU  KATIKA
USO WA YESU KRISTO..
Na hii ndio kazi ya Mafundisho ya Neno la MUNGU yanapopita mahali popote, na ndio  kazi  kubwa  ya  Huduma  ya  Ualimu  ndani  ya  Kanisa  nalo  ndilo  tunalihitaji pia kutoka kwa MUNGU atusaidie kufundisha mafundisho yafaayo kuwapa watu Elimu ya MUNGU. Naam na iwe hivyo kwa Huduma zote za Ualimu.
Tuaminivyo:
Ø  Kama Huduma Tunaamini katika MUNGU Baba, Mwana na Roho Mtakatifu (UTATU MTAKATIFU)

Ø  Tunaamini ya kwamba YESU ALIKUFA MSALABANI NA SIKU YA TATU ALIFUFUKA KUTOKA KWA WAFU NA YU HAI MILELE na ya kwamba ATATUFUFUA nasi siku ya mwisho.

Ø  Tunaamini WOKOVU WA MWANADAMU unapatikana kwa KIFO CHA YESU MSALABANI.

Ø  Tunaamini katika Biblia (Maandiko Matakatifu) yenye Vitabu 66 kama msingi wa Mafundisho yetu.

Ø  Tunaamini WATU TULIOOKOKA tumepewa Jukumu la kuwaeleza watu wote na Ulimwenguni Kote habari Njema za Msamaha wa Dhambi kwa Kumwamini BWANA YESU KRISTO.

Huduma tunazofanya:
Huduma ya NURU hufanya huduma mbalimbali ambazo lengo lake ni kufikisha mafundisho ya Neno la MUNGU kwa watu wote wenye uhitaji wa mafundisho. Katika kutenda hilo Huduma ya NURU hufanya kazi zifuatazo;

SEMINA:  hujumuisha semina za kuandaliwa na Makanisa na makundi mbalimbali na zile za kuandaa wenyewe (yaani Huduma ya NURU)

MAKONGAMANO: Ni mafundisho maalumu kwa makundi maalumu, kama vile wafanyabiashara, wanafunzi, viongozi n.k

MAFUNDISHO KWA NJIA YA MTANDAO: Pia tunafanya mafundisho kwa njia ya mtandao, hapa hujumuisha mitandao ya Kijamii, tovuti na Barua pepe na pia kwa simu za mikononi kwa njia ya Whatsap na sms.

MAFUNDISHO KWA VIDEO NA AUDIO: Pia yapo mafundisho kwa njia ya video na audio (kusikiliza) ili kwa wale ambao hawajawahi kuhudhuria Semina zetu au makongamano basi wanaweza kufanikiwa kupata mafundisho hayo kwa njia hizo. 

No comments:

Post a Comment

Home