+255 753 204 743 mkumbosj@gmail.com, facebook.com/mwlsamwelmkumbo

Tuesday, April 2, 2013


Mwl; Samwel Mkumbo


Divai MPYA!!!!!!!!!!

Ni wazi kabisa ya kuwa katika mabadiliko ya nyakati hasa za ulimwengu yapo mambo mengi sana ambayo tunahitaji kujifunza sana huku tukitazama namna ya kuendana na mabadiliko hayo.
Hakuna mtu atiaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu; maana kile kilichotiwa huondoa kipande cha lile vazi, na pale palipotatuka huzidi. Wala watu hawatii divai mpya katika viriba vikuukuu; na kama wakitia, vile viriba hupasuka, divai ikamwagika, na viriba vikaharibika; bali hutia divai mpya katika viriba vipya, vikahifadhika vyote…,..,.. (Math 9:16-17)
Japokuwa watu wamekuwa wakitumia mstari huu kujaribu kuhalalisha mabadiliko HASI yanayoingia katika kanisa na hata kufikia kuona Ndio mwelekeo Halali wa kanisa hasa kwa vijana na kuona kuwa  ni “Divai mpya”  na wao ni “viriba vipya”(vijana).

Lakini hiyo haikuwa maana ya Yesu katika mfano huo maana alichokuwa anakionesha ni namnagani walivyotakiwa kuenenda hao mafarisayo wanaotii sheria na wale wanaomtii Kristo yaani wale waaminio wokovu huja kwa neema ya Kristo. Tazama hapa;
Wakati ule wanafunzi wake Yohana wakamwendea, wakasema, Kwa nini sisi na Mafarisayo twafunga, bali, bali wanafunzi wako hawafungi?......(Math 9:14)
Tunachoweza kuona hapo ni juu ya suala la wanafunzi wa Yohana kutaka kufananisha nyakati za Yohana na Yesu pasi kujua mabadiliko ya nyakati na YESU aliwapa mfano ambao ulikuwa ni jawabu la ndani ya mioyo na fumbo la Imani,.

Naam, kinachotazamwa hapo ni namna ambavyo wanafunzi wa Yohana hawakujua hali iliyopo ndani ya Ukristo, naam hata yale mafundisho hayakuwa katika namna ambavyo wangeelewa kwa haraka kwa jinsi ya kawaida, kwao haikuwa rahisi kujibadili na kujua Neema iliyopo katika Kristo, bali walitaka kuona ni kwa namna gani wanaweza kuwasaidia wanafunzi wa Yesu ili nao wapate kushika mapokeo.
Lakini Tito aliyekuwa pamoja name, naye ni Myunani, hakulazimishwa kutahiriwa. Bali kwa ajili ya ndugu za uongo walioingizwa kwa siri ili kuupeleleza uhuru wetu tulionao katika Kristo Yesu, ili watutie utumwani..,,..,,.. (Wagalatia 2:3-4)

Katika kutazama hapo utagundua ya kuwa hao wanafunzi wa Yohana walichunguza uhuru wa wanafunzi walionao katika Kristo ndiposa wakaja na hoja au ushauri kwao, lakini jawabu la Yesu linatupa kuona ni kwa jinsi gani ilivyo vigumu kwa watu walio katika mlengo Fulani wa imani au wanaoshikilia msimamo Fulani wa Imani inavyokuwa ni vigumu kuishi katika mfumo mwingine wa imani.
Na kama ukisoma vizuri mistari ile ya Mathayo, ule mtari wa 16 unaendana na Yohana 1:17 unaosema hivi; …. Kwa kuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo…..

Ndiposa waweza kuona hao walioishi kwa Sheria basi watahukumiwa kwa sheria na hao walioishi kwa Neema naam nao watahukumiwa kwa Neema.

Basi Divai MPYA huwekwa katikaviriba vipya maana ni yenye nguvu tena uhitaji mahali penye uwezo wa kutunza maana viriba vya kale vimechoka kwa kujaza divai iliyoisha ukali wake kwa kukaa muda mrefu na kupoteza ladha yake tena huwa ni kama kuweka kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu maana hata rangi na mng’ao wake hutofautiana sana na hilo ndilo alilokuwa analisemaBwanaYesu hasa katika kujua nafasi ya jambo jipya na ndio maana sisi hatuwezi kumbeba Kristo katika miili yetu hii iliyochoka na kuchakaa hasa miili yenye taabu na majuto.
Tunahitaji kubadilishwa kwanza na kuwa watu wapya kabisa.   

No comments:

Post a Comment

Home