+255 753 204 743 mkumbosj@gmail.com, facebook.com/mwlsamwelmkumbo

Friday, May 31, 2013

SIRI YA KUWA NA FURAHA KATIKA KRISTO

Mwl; Emmanuel Mollel

Kristo asifiwe. Ninamshukuru sana Mungu kwa ajili yako wewe msomaji wa ujumbe huu kwa nafasi ambayo Mungu anaendelea kukupa Maishani Mwako. Zab 118:24 (Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana nasi tutaifurahia.) Furaha ni mwonekano unaoanzia ndani ya mtu hata kuonekana nje kutokana na vile aonavyo ndani yake. Hivyo furaha ni jambo lililo chini ya uamuzi wako. Biblia inasema kila siku aliyoifanya Bwana ni ya furaha.Maana yake unapoamka asubuhi na kukiri maneno haya haijalishi utakutana na nini lakini Mungu ataitunza furaha yako. Shetani anachotamani ni wewe usiwe na furaha maishani mwako. Asante Bwana Yesu uliyetupa siku mzuri ili tufurahi. Furaha inakuja kwa mambo makuu matatu. 

1. Ukiri wa kinywa chako kwamba utakuwa na furaha.

 2. Imani kwa Mungu wako akupaye furaha. 

3.Kuikubali siku hii kwamba imetoka kwa Bwana.

 Ukifanya hivyo haijalishi kitu gani kimetokea kwako, kizuri au kibaya Mungu atashughulika. Utakuwa huru kila utakapokuwa. Yohana 8:36. Basi mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli








No comments:

Post a Comment

Home