+255 753 204 743 mkumbosj@gmail.com, facebook.com/mwlsamwelmkumbo

Thursday, September 4, 2014

HUZUNI YA JINSI YA MUNGU (SEHEMU YA PILI)

GOMBO LA WIKI
Na:  Samwel Mkumbo



















Sehemu ya 2.
“HUZUNI YA JINSI YA  MUNGU”
Katika wiki hii tunaendelea na mtiririko wa kujifunza somo linaloitwa “HUZUNI YA JINSI YA MUNGU”, na wiki iliyopita tulijifunza mambo kadhaa, na mstari wetu mkuu tunaoutumia katika Somo hili ni ule wa     2 Wakorintho 7:10 na katika huo tutajifunza mengi zaidi……..
KARIBU!!
2 Wakorintho 7:10, umeandikwa hivi;
“Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti.”
Kujutia dhambi.
Ili mtu aweze kujutia dhambi  ni lazima  kuwepo na mguso wa ndani ya moyo (nafsi yake), lakini hii si hatua ya mwisho, maana wengi wanapotoka hatua ya kwanza (Kutambua Kosa) huwa wanaishia kwenye hii hatua ya pili ya “Kujutia” lile alilolitambua kuwa ni kosa ndani yake na huwa wanaishia hapo,
Luka 15:17 utakuta maneno haya:-
Alipozingatia moyo mwake  alisema ……………….. “mwana mpotevu hakuwa na cha kufanya baada ya kutambua dhambu yake ila kwanza kujutia moyoni”. NA HATUWEZI KUJUTIA DHAMBI BILA YAKUITAMBUA DHAMBI.  Sasa baada ya hatua hii ya kujutia dhambi ambayo inatokana na Kutambua Dhambi kuna hatua nyingine zaidi zinazofuata mbele baada ya hapo.
Kabla sijaendelea jikumbushe tulipoanzia na pia utambue kuwa tunajifunza kuhusu “HUZUNI YA JINSI YA MUNGU”.
Kukiri dhambi.
Ni hali kuwa kukubali kuwa lile ulilofanya ni dhambi/kosa na kuwa wazi ya kuwa nawe watambua kuwa ni kosa, kuna shida kwa watu wengi sana ya kutokubali kukosea na kama wamekosea huwa na mawazo ya kila namna ya kufanya lile walilotenda kuwa si kosa na hivyo HUJARIBU KUJITETEA, na katika kujitete huko ndiko huleta makosa zaidi.
Kielelezo: Habari za Adamu kumkosea MUNGU na namna alivyotafuta kujitetea, tukisoma katika kitabu cha Mwanzo 3:11-12 inasema hivi;
11Akasema, Ni nani aliyekuambia ya kuwa u uchi? Je! Umekula wewe matunda ya mti niliyokuagiza usiyale? 12 Adamu akasema, Huyo mwanamke uliyenipa awe pamoja nami ndiye aliyenipa matunda ya mti huo, nikala.
Katika mistari hiyo hapo juu utagundua namna mtu anayejaribu kukwepa kukiri kosa alilolifanya kunavyoweza kuleta madhara, maana swali alilouliza MUNGU na jibu alilojibu Adamu ni tofauti lakini hii inatokana na kutokuwa na moyo wa kukiri kosa,. Tazama nami hivi;
…….. Je! Umekula wewe matunda ya mti niliyokuagiza usiyale? Hili lilikuwa ni swali la Mungu kwa Adamu kutokana na kuambiwa kwamba yu uchi.
………Adamu akasema, HUYO MWANAMKE ULIYENIPA awe pamoja nami ndiye aliyenipa matunda… hili ndilo lilikuwa ni jibu la Adamu baada ya kuulizwa na MUNGU kama amekula matunda ya mti aliyokatazwa asile.
Tazama nami: Baada ya Adamu kula tunda alilokatazwa asile papo hapo ALITAMBUA KOSA/DHAMBI aliyokuwa amefanya na moyoni mwake akaanza kujutia kile lichokuwa amefanya.
 Na hili linaonekana katika Mwanzo 3:7 inasema hivi;
“Wakafumbuliwa macho wote wawili wakajijua kuwa wa uchi, wakashona majani ya mtini, wakajifanyia nguo.” Ukitazama hapo utaona neno WAKAFUMBULIWA MACHO WOTE WAWILI…… ikiwa na maana baada tu ya kula tunda “Wakatambua ya kuwa wamekosea” maana waliona matokeo ya kile walichokifanya papo hapo na ndio maana wakajificha machoni pa Mungu.
Hivyo basi Adamu ndani yake alikuwa ameshavuka hatua ya kwanza ya KUTAMBUA KOSA/DHAMBI, lakini pia katika hatua hiyo tunaona na suala lingine ya kwamba Adamu ALIJUTIA KOSA/DHAMBIA aliyofanya na ndio maana tunaona suala la Mahangaiko linatokea, kwa maana ilibidi waanze kutafuta namna ya” Kujisitiri Utupu wao” maandiko yananena “…..wakashona majani ya mtini, wakajifanyia nguo.”
Labda nikujulishe hili japo nitakueleza kwa undani zaidi huko mbele tunapoendelea kujifunza ya kwamba Hatua ya KUJUTIA KOSA/DHAMBI huja na maangaiko ya ndani na nje. Na ndio maana ule mstari wa 2Wakorintho 7:10 kuna maneno yanayosema bali huzuni ya dunia hufanya mauti.”, lakini pia nikuongezee maarifa kwa kukueleza ya kwamba moja ya jambo lililo karibu na Mahangaiko ni “Mauti” hivyo inapotokea mtu akatenda kosa halafu ndani yake ikaingia roho ya mahangaiko inayotokana na Kutambua na Kujutia Kosa kunahitajika Nguvu ya Mungu inayokuja kwa njia ya Huzuni ili kumfanya AKIRI KOSA NA KUTUBU.
Nitakuambia kwa kirefu baadae, lakini ni hivi; kwa hali ya kawaida mwanadamu mwenyewe ni kazi kujipeleka katika hatua ya KUKIRI NA KUTUBU KOSA/DHAMBI bali huwa anaishia katika hatua ya KUTAMBUA NA KUJUTIA, na tatizo kubwa ni kwamba kama mtu anaishia kwenye kujuta tu basi yale majuto yasipokutana na “HUZUNI YA JINSI YA MUNGU” ambayo inapelekea mtu Kukiri  na Kutubu basi mauti huwa inachukua nafasi.
Zaburi 32:5b tunasoma:-      
Nalisema nitayakiri maovu yangu kwa BWANA,
Nawe ukanisamehe upotevu wa dhambi yangu.
Tazama nami:
 Kukiri dhambi huwa nje ya mtu na hutokana na kujutia dhambi kunakofanyika ndani ya mtu.
2 samweli 12:13 tunakuta nmaneno haya;
“Daudi akamwambia Nathani, Nimemfanyia Bwana dhambi……………….. mfalme Daudi alipotambua kosa alilolifanya na kulijutia ndani yake alikiri mbele ya nabii nathani ya kuwa Amemfanyia Bwana dhambi. Hakukaa kimya wala hakutaka kumsingia mkewe Huria kuwa alikuwa amesababisha kwa kosa la kuoga nje mchana. Naam! Angeweza tu kurudisha kosa kwa mkewe Huria kama alivyofanya Adamu kwa kusema “Ni huyu mwanamke uliyenipa….” Maana anataka kumtuhumu Mungu kwamba asingempa huyo mwanamke basi asingekula tunda.
Lakini Daudi yeye alikiri kabisa ya kwamba amemfanyia Mungu  dhambi na alikubali na hiyo inatokana na matokeo ya kujutia dhambi kulikotokea ndani ya Daudi. Na hii ni kwa sababu “HUZUNI YA JINSI YA MUNGU” iliingia ndani ya Daudi ambayo inamtoa kwenye Hatua ya Kutambua Kosan a Kujutia na hiyo huzuni inampeleka kwenye KUKIRI hilo kosa pia.
Itaendelea………………………………………………….
Mungu awe pamoja nawe katika wiki hii unapotafakari GOMBO LA WIKI.  
DOWNLOAD HERE

No comments:

Post a Comment

Home